Swali: Inajuzu kufunga siku sita za Shawwaal kabla ya mtu kulipa deni lake la Ramadhaan?
Jibu: Wanachuoni wametofautiana katika hilo. Usawa ni kwamba jambo lililowekwa katika Shari´ah ni kutanguliza kwanza deni kabla ya kufunga zile siku sita za Shawwaal na Sunnah nyenginezo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”[1]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Atakayetanguliza siku sita kabla ya kulipa hakuifuatishia Ramadhaan. Ameifuatanishia baadhi ya siku za Ramadhaan. Jengine ni kwamba kulipa deni ni faradhi. Kufunga faradhi kuna haki zaidi ya kupewa umuhimu.
[1] Muslim (1164), at-Tirmidhiy (759), Abu Daawuud (2433), Ibn Maajah (1716), Ahmad (05/417) na ad-Daarimiy (1754).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/392)
- Imechapishwa: 09/06/2018
Swali: Inajuzu kufunga siku sita za Shawwaal kabla ya mtu kulipa deni lake la Ramadhaan?
Jibu: Wanachuoni wametofautiana katika hilo. Usawa ni kwamba jambo lililowekwa katika Shari´ah ni kutanguliza kwanza deni kabla ya kufunga zile siku sita za Shawwaal na Sunnah nyenginezo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”[1]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Atakayetanguliza siku sita kabla ya kulipa hakuifuatishia Ramadhaan. Ameifuatanishia baadhi ya siku za Ramadhaan. Jengine ni kwamba kulipa deni ni faradhi. Kufunga faradhi kuna haki zaidi ya kupewa umuhimu.
[1] Muslim (1164), at-Tirmidhiy (759), Abu Daawuud (2433), Ibn Maajah (1716), Ahmad (05/417) na ad-Daarimiy (1754).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/392)
Imechapishwa: 09/06/2018
https://firqatunnajia.com/inatakiwa-kutanguliza-deni-kwanza-kabla-ya-swawm-ya-shawwaal/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)