Inajuzu kwa mume aliyetoka safarini kumwingilia mke wake Ramadhaan?

Swali: Inajuzu kwa mtu kumwingilia mke wake baada ya kuoga pindi atapofika nyumbani kwake kutoka safarini hali ya kuwa si mwenye kufunga na baada ya kujizuia na kula na kunywa akamkuta mke wake anajisafisha na hedhi?

Jibu: Msafiri akifika katika mji wake katika Ramadhaan anachotakiwa ni yeye kujizuia na kula na kunywa. Haijuzu kwake kumwingilia mke wake siku hiyo aliyofika kwa kuzingatia utukufu wa zama za funga.

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (10/316-317)
  • Imechapishwa: 17/06/2017