Swali: Ni ipi hukumu ya wanawake kuyatembelea makaburi? Kusemwe nini kuhusu kitendo cha ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ya kwamba alitembelea kaburi la kaka yake?

Jibu: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi sana. Upokezi mmoja umetaja tu ya kwamba amewalaani wanawake wenye kuyatembelea makaburi. Kwa hivyo haijuzu kwa yeyote, si ´Aaisha wala mwengineo. Lakini huenda Hadiyth haikumfikia (Radhiya Allaahu ´anhaa).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (66) http://alfawzan.af.org.sa/node/16524
  • Imechapishwa: 13/08/2017