Swali: Nimesoma kitabu “Haadi al-Arwaah” kuhusu I´tiqaad ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ya kwamba imani ni kauli na ´amali, inazidi na kupungua na hawasemi kuwa imeumbwa au haikuumbwa. Vipi hili?

Jibu: Kuna faida gani ya kusema imani imeumbwa au haikuumbwa? Kuna haja yepi ya hili? Huku ni kujikalifisha. Salaf hawakuwa wanasema kama imani imeumbwa au haikuumbwa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (11) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_11.mp3
  • Imechapishwa: 20/06/2018