Swali: Sisi tuko na imamu wetu ambaye hivi sasa anaswalisha hali ya kukaa kwenye kiti kwa sababu ya utuuzima na maamuma wanaswali nyuma yake kwa kusimama.

Jibu: Haijuzu kufanya hivi. Imamu huyu ni mjinga. Vipi atawaswalisha watu ilihali amekaa na isitoshe tatizo lake ni lenye kudumu lisilotarajiwa kuondoka? Imamu ambaye amepangwa ikiwa kuna matarajio ya kumalizika tatizo lake ambapo akaswali kwa kukaa ndiye ambaye maamuma pia wanatakiwa kuswali nyuma yake kwa kukaa. Imamu akiwa ndiye amepangwa kwenye msikiti huo na kukawa kuna matarajio ya kumalizika tatizo lake ambapo akaswali kwa kukaa ndiye ambaye maamuma pia wanatakiwa kuswali kwa kukaa. Ama huyu anaswali kwa kukaa kwenye kitu na ni mwenye kuendelea kufanya hivo na isitoshe tatizo lake silo la kutarajia kuisha, haifai kufanya hivo. Ni nani amempa fatwa ya kufanya hivo? Ni wajibu kwa kamati ya msikiti wamzuie kuswalisha.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (66) http://alfawzan.af.org.sa/node/16524
  • Imechapishwa: 13/08/2017