Swali 112: Kuna wenye kusema kwamba watawala na wanachuoni wa nchi hii wameitokomeza Jihaad, jambo ambalo ni kumkufuru Allaah. Ni yepi maoni yako katika maneno yake?

Jibu: Haya ni maneno ya mjinga. Bali yanaonyesha kuwa hana uelewa wala elimu na kwamba anawakufurisha watu. Haya ni maoni ya Khawaarij. Wao wanapita juu ya maoni ya Khawaarij na Mu´tazilah. Tunamuomba Allaah afya. Lakini hatuwajengei dhana mbaya. Bali tunasema kuwa watu hawa ni wajinga. Ni lazima kwao kusoma kabla ya kuzungumza. Ama wakiwa na elimu kisha wakazungumza maneno haya, basi itambulike kuwa haya ni maoni ya Khawaarij na wapotevu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa ´Ulamaa-ul-Kibaar fiy al-Irhaab wat-Tadmiyr, uk. 302-303
  • Imechapishwa: 19/10/2019