Ihyaa’ at-Turaath na ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq ni Hizbiyyuun

Da´wah ya jumuiya ya Ihyaa´ at-Turaath, inayoongozwa na ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq, ni Da´wah ya Hizbiyyah. Haijali kusambaza dini na kulingania katika dini. Inajali sana kupata watu. Mmoja wao – na mimi namhimidi Allaah juu ya hilo – ya kwamba Da´wah yao haitopata kidato Yemen maadamu Muqbil yupo. Ni kweli. Ni kweli ameona upeo wa mbali. Ni wingi wa pesa ngapi wameshakuja nazo! Ni kama kwamba wanazitupa kwenye kisima. Hata hivyo mbali na upungufu wake mwanzoni ilikuwa ni Da´wah ya Salafiyyah. Kulikuwa mzozano baina yao na baina ya al-Ikhwaan al-Muslimuun. Mwanzoni Shaykh al-Albaaniy alikuwa akimtetea ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq kwa kuwa wakati huo alikuwa hajaonesha Uhizbiyyah wake. Baada ya hapo mambo yake yakadhihirika tokea wakati baadhi ya ndugu zetu wa al-Madiynah walipoenda Kuwait. Hapo ndipo akaanza kutetea Televisheni, kuwazingatia ndugu zake al-Madiynah kuwa ni Khawaarij, akaandika kitabu kinachoitwa “al-Walaa´ wal-Baraa´”, ukweli wa mambo ni kuwa, al-Walaa´ (kupenda) mahakama, al-Baraa (kuchukia na kujiweka mbali) na Madu´aat wanaolingania katika dini ya Allaah.

  • Mfasiri: Firqatunnajia.com