Ibn ´Uthaymiyn kuhusu kurekodi kwa video camera mawaidha ya dini

Swali: Ni ipi hukumu ya kuchukua mihadhara na semina kwa kutumia kifaa cha video camera?

Jibu: Naona kuwa hakuna ubaya kurekodi mihadhara na semina kwa kifaa cha video camera haja ikipelekea kufanya hivo au manufaa yakapelekea kufanya hivo kutokana na yafuatayo:

La kwanza: Kurekodi ambako ni moja kwa moja (live) hakuingii katika kuiga uumbaji wa Allaah. Hilo liko wazi kwa wale wenye kuzingatia.

La pili: Picha haionekani kwenye mkanda. Kwa hivyo hakuna kitendo cha kuhifadhi picha.

La tatu: Tofauti iliyopo ya kuingia video camera katika kuiga uumbaji wa Allaah – hata kama hilo linarithisha kufanana – hakika haja au manufaa yaliyohakikiwa hayafanyi tofauti kuisha katika jambo ambalo haijabaini namna ya kukatazwa kwake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (02/284)
  • Imechapishwa: 03/07/2017