Swali: Ni ipi hukumu ya mfungaji kutumia sprei mchana wa Ramadhaan kwa sababu ya maradhi ya pumu na mfano wake?

Jibu: Hukumu yake ni kufaa iwapo atalazimika kufanya hivo. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:

وَقَدْ فَصَّلَ لَكُم مَّا حَرَّمَ عَلَيْكُمْ إِلَّا مَا اضْطُرِرْتُمْ إِلَيْهِ

“… na ilhali ameshakubainishieni yale Aliyokuharamishieni isipokuwa vile mlivyofikwa na dharura navyo.” (06:119)

Jengine ni kwa sababu hilo halifanani na kula na kunywa. Hilo limefanana na kuchota damu kwa sababu ya kipimo au sindano isiyokuwa ya lishe.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://www.sahab.net/forums/index.php?app=forums&module=forums&controller=topic&id=84940
  • Imechapishwa: 20/05/2018