Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema ndani ya swalah kuhusu Mtume:
اللهم صل على محمد طبّ القلوب و دوائها
“Ee Allaah! Mswalie Muhammad ambaye ni tiba na dawa ya mioyo”?
Jibu: Maneno haya si sahihi. Ni maneno ya kijumla. Kusema kwamba ni tiba na dawa ya mioyo ni maneno ya kijumla. Tiba na dawa ya mioyo ni kwa kufuata Shari´ah. Haya yanaweza kumfanya mtu akaelewa kwamba yeye ndiye anatibu na ni dawa kwa nafsi yake mwenyewe na kwamba ananufaisha na anadhuru. Maneno haya si sahihi. Wafunzeni watu matamshi sahihi:
اللهم صل على محمد و على آل محمد كما صليت على آل إبراهيم
“Ee Allaah! Msifu Muhammad na jamaa zake Muhammad kama Ulivyomsifu Ibraahiym… ”
Au:
اللهم صل على النبي الأمي
“Ee Allaah! Msifu Mtume ambaye si msomi…”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 49
- Imechapishwa: 20/06/2019
Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema ndani ya swalah kuhusu Mtume:
اللهم صل على محمد طبّ القلوب و دوائها
“Ee Allaah! Mswalie Muhammad ambaye ni tiba na dawa ya mioyo”?
Jibu: Maneno haya si sahihi. Ni maneno ya kijumla. Kusema kwamba ni tiba na dawa ya mioyo ni maneno ya kijumla. Tiba na dawa ya mioyo ni kwa kufuata Shari´ah. Haya yanaweza kumfanya mtu akaelewa kwamba yeye ndiye anatibu na ni dawa kwa nafsi yake mwenyewe na kwamba ananufaisha na anadhuru. Maneno haya si sahihi. Wafunzeni watu matamshi sahihi:
اللهم صل على محمد و على آل محمد كما صليت على آل إبراهيم
“Ee Allaah! Msifu Muhammad na jamaa zake Muhammad kama Ulivyomsifu Ibraahiym… ”
Au:
اللهم صل على النبي الأمي
“Ee Allaah! Msifu Mtume ambaye si msomi…”
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 49
Imechapishwa: 20/06/2019
https://firqatunnajia.com/ibn-baaz-kusema-kwamba-mtume-ni-tiba-na-dawa-ya-mioyo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)