Ibn Baaz kuhusu ujinga ni udhuru IX

Swali: Tofauti iliopo juu ya kumpa udhuru mjinga ni miongoni mwa mambo ambayo wanachuoni wametofautiana?

Jibu: Ni masuala makubwa. Msingi ni kwamba hapewi udhuru yule ambaye anaishi kati ya waislamu. Yule aliyefikiwa na Qur-aan na Sunnah hapewi udhuru. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:

هَـٰذَا بَلَاغٌ لِّلنَّاسِ

“Hii ni ufikishwaji wa ujumbe kwa watu.” (14:52)

وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَـٰذَا الْقُرْآنُ لِأُنذِرَكُم بِهِ وَمَن بَلَغَ

“Nimefunuliwa Wahy hii Qur-aan ili nikuonyeni kwayo na kila itakayomfikia.” (06:19)

 Ambaye kafikiwa na Qur-aan na Sunnah si mwenye kupewa udhuru. Yaliyomfikia ni kutokana na kufanya kwake mchezo na kutokujali.

Swali: Lakini mtu anaweza kusema kwamba ni miongoni mwa mambo ambayo wanachuoni wametofautiana?

Jibu: Hapana, hakuna tofauti. Isipokuwa katika mambo nyeti ambayo kweli yanaweza kujificha. Kama mfano wa kisa cha yule aliyewaambia watu wake: “Nichomeni moto.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat (01) http://ajurry.com/safrawy/chorohat-elakida/charh-kachef-chobohat/charh-ibn-baz/01.mp3
  • Imechapishwa: 29/03/2019