Ibn Baaz kuhusu shairi la al-Burdah

Makusudio ya haya yote ni kufunga njia zote ziwezazo kuwapelekea watu kuchukulia wepesi shirki. Wakitumia maneno kama “bwana” na mfano wake katika upetukaji ambayo yanatumiwa na watu hii leo matokeo yake yanaweza kuwafanya wakaanza kumwabudu badala ya Allaah, wakamuomba, wakamtaka msaada, kudai kwamba anajua mambo yaliyofichikana na mfano wake. Kama alivosema mwandishi wa “al-Burdah” wakati aliposema:

Ee kiumbe mbora! Sina mwengine zaidi yako wa kumkimbilia wakati wa majanga

Usiponitukuza siku ya Qiyaamah na ukanishika mkono, nimeangamia.

Katika ukarimu wako ni pamoja na dunia hii na mali zake

na miongoni mwa elimu zako ni pamoja na elimu ya Ubao na Kalamu.

Kuvuka mipaka kulimpelekea akasema kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ndiye ambaye atamwokoa siku ya Qiyaamah na kwamba yule ambaye hatookolewa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi ameangamia. Huu ni upetukaji mkubwa. Amesema vilevile kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anayajua yaliyomo katika Ubao na katika Kalamu na kwamba yeye anakijua kila kitu.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 181-182
  • Imechapishwa: 15/11/2018