Swali: Vipi kumtolea adhaana kuliani mwa sikio la mtoto na kumkimia kushotoni mwa sikio?
Jibu: Haya yamewekwa katika Shari´ah kwa mujibu w kundi la wanachuoni. Ni jambo limepokelewa katika baadhi ya Hadiyth ambazo katika cheni zake kuna maneno. Muumini akifanya hivo ni vizuri. Kwa sababu ni miongoni mwa Sunnah na mambo ya kujitolea. Katika cheni ya wapokezi kuna mpokezi anayeitwa ´Aaswim bin ´Ubaydillaah bin ´Aaswim bin ´Umar bin al-Khattwaab na ana udhaifu. Lakini ina mapokezi mengine yenye kuitolea ushahidi. Mtume (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) alimpa jina mwanae ´Ibraahiym` na haikuhifadhiwa kwamba alimtolea adhaana kwenye sikio lake la kulia na kumkimia kwenye sikio lake la kushoto. Kadhalika wale watoto wa Answaar ambao alikuwa akiletewa ili awafanyie Tahniyq na awape majina. Sijaona kuwa aliwatolea adhaana na kuwakimia masikioni. Lakini muumini akifanya hivo kutokana na ile Hadiyth tuliyoashiria hakuna neno. Lakini zinapeana nguvu baadhi kwa zengine. Ni jambo jepesi. Endapo mtu atafanya ni vizuri kutokana na Hadiyth zinazopeana nguvu. Asipofanya pia hakuna neno.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/7045/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%A7%D9%84%D8%A7%D8%B0%D8%A7%D9%86-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D8%AD%D8%AF%D9%89-%D8%A7%D8%B0%D9%86%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D9%85%D9%88%D9%84%D9%88%D8%AF-%D9%88%D8%A7%D9%84%D8%A7%D9%82%D8%A7%D9%85%D8%A9-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D8%A7%D8%AE%D8%B1%D9%89
- Imechapishwa: 14/06/2019
Swali: Vipi kumtolea adhaana kuliani mwa sikio la mtoto na kumkimia kushotoni mwa sikio?
Jibu: Haya yamewekwa katika Shari´ah kwa mujibu w kundi la wanachuoni. Ni jambo limepokelewa katika baadhi ya Hadiyth ambazo katika cheni zake kuna maneno. Muumini akifanya hivo ni vizuri. Kwa sababu ni miongoni mwa Sunnah na mambo ya kujitolea. Katika cheni ya wapokezi kuna mpokezi anayeitwa ´Aaswim bin ´Ubaydillaah bin ´Aaswim bin ´Umar bin al-Khattwaab na ana udhaifu. Lakini ina mapokezi mengine yenye kuitolea ushahidi. Mtume (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) alimpa jina mwanae ´Ibraahiym` na haikuhifadhiwa kwamba alimtolea adhaana kwenye sikio lake la kulia na kumkimia kwenye sikio lake la kushoto. Kadhalika wale watoto wa Answaar ambao alikuwa akiletewa ili awafanyie Tahniyq na awape majina. Sijaona kuwa aliwatolea adhaana na kuwakimia masikioni. Lakini muumini akifanya hivo kutokana na ile Hadiyth tuliyoashiria hakuna neno. Lakini zinapeana nguvu baadhi kwa zengine. Ni jambo jepesi. Endapo mtu atafanya ni vizuri kutokana na Hadiyth zinazopeana nguvu. Asipofanya pia hakuna neno.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/7045/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D8%A7%D9%84%D8%A7%D8%B0%D8%A7%D9%86-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D8%AD%D8%AF%D9%89-%D8%A7%D8%B0%D9%86%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D9%85%D9%88%D9%84%D9%88%D8%AF-%D9%88%D8%A7%D9%84%D8%A7%D9%82%D8%A7%D9%85%D8%A9-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D8%A7%D8%AE%D8%B1%D9%89
Imechapishwa: 14/06/2019
https://firqatunnajia.com/ibn-baaz-kuhusu-kumuadhini-na-kumkimia-mtoto-mchanga/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)