al-Khaliyliy amesema:
“Kuhusu dalili za kinakili – za wanaopinga kuonekana kwa Allaah – baadhi zinapatikana katika Qur-aan na zingine katika Sunnah.”[1]
Kisha akasema:
“Katika Qur-aan ni maneno Yake (Ta´ala):
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[2]
Halafu akasema:
“Dalili hapa ni kwamba (Ta´ala) amejisifu kuwa macho hayamdiriki. Kudiriki maana yake ni kuona. Ikapata kubainika kuwa kutoonekana kwa macho ni sifa ya kidhati yenye kulazimiana Naye (Ta´ala). Lau kungelikuwa kipindi anaonekana basi kujisifu Kwake kungeondoka na mambo yakishakuwa hivo inageuka kuwa kinyume chake ambacho ni kulaumika – Allaah ametakasika na hilo.”
Akaendelea kusema:
“Kwa upande mwingine ni kwamba [hapa] Allaah anaelezea sifa miongoni mwa sifa Zake na maelezo ya Allaah hayabadiliki. Lau ingelibadilika basi kubadilika kwake ingelikuwa ni kumkadhibisha:
وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ قِيلًا
“Na nani aliye mkweli zaidi kwa kauli kuliko Allaah?”[3]
Wacha nikupe maneno ya wahakiki walivyoifasiri Aayah katika mambo yafuatayo:
Mosi: Kubainisha kuwa katika makanusho matupu hakuna matapo ndani yake, kama anavyoonelea al-Khaliyliy.
Pili: Kubainisha tofauti kati ya “kudiriki” na “kuona”.
Kuhusu tafsiri ya Aayah tumeshatangulia kunukuu kutoka katika Tafsiyr ya Ibn Jariyr kupitia kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) aliyefasiri:
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[4]
“Macho hayamzunguki.”
Qataadah amesema:
“Ni mkubwa zaidi kwa macho kuweza kumzunguka.”
´Atwiyyah al-´Awfiy amesema:
“Watamtazama Allaah na macho yao hayatoweza kumzunguka kutokana na ukubwa Wake. Lakini Yeye macho Yake yanawazunguka.” Hiyo ndio maana ya maneno Yake:
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[5]
Kuhusu makanusho matupu hakuna matapo ndani yake tofauti na anavyoonelea al-Khaliyliy na maimamu wake Jahmiyyah, Mu´tazilah na Imaamiyyah katika mlango huu.
[1] Uk. 68
[2] 06:103
[3] 04:122
[4] 06:103
[5] 06:103
- Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Radd al-Qawiym, uk. 99-100
- Imechapishwa: 14/01/2017
al-Khaliyliy amesema:
“Kuhusu dalili za kinakili – za wanaopinga kuonekana kwa Allaah – baadhi zinapatikana katika Qur-aan na zingine katika Sunnah.”[1]
Kisha akasema:
“Katika Qur-aan ni maneno Yake (Ta´ala):
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[2]
Halafu akasema:
“Dalili hapa ni kwamba (Ta´ala) amejisifu kuwa macho hayamdiriki. Kudiriki maana yake ni kuona. Ikapata kubainika kuwa kutoonekana kwa macho ni sifa ya kidhati yenye kulazimiana Naye (Ta´ala). Lau kungelikuwa kipindi anaonekana basi kujisifu Kwake kungeondoka na mambo yakishakuwa hivo inageuka kuwa kinyume chake ambacho ni kulaumika – Allaah ametakasika na hilo.”
Akaendelea kusema:
“Kwa upande mwingine ni kwamba [hapa] Allaah anaelezea sifa miongoni mwa sifa Zake na maelezo ya Allaah hayabadiliki. Lau ingelibadilika basi kubadilika kwake ingelikuwa ni kumkadhibisha:
وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللَّـهِ قِيلًا
“Na nani aliye mkweli zaidi kwa kauli kuliko Allaah?”[3]
Wacha nikupe maneno ya wahakiki walivyoifasiri Aayah katika mambo yafuatayo:
Mosi: Kubainisha kuwa katika makanusho matupu hakuna matapo ndani yake, kama anavyoonelea al-Khaliyliy.
Pili: Kubainisha tofauti kati ya “kudiriki” na “kuona”.
Kuhusu tafsiri ya Aayah tumeshatangulia kunukuu kutoka katika Tafsiyr ya Ibn Jariyr kupitia kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) aliyefasiri:
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[4]
“Macho hayamzunguki.”
Qataadah amesema:
“Ni mkubwa zaidi kwa macho kuweza kumzunguka.”
´Atwiyyah al-´Awfiy amesema:
“Watamtazama Allaah na macho yao hayatoweza kumzunguka kutokana na ukubwa Wake. Lakini Yeye macho Yake yanawazunguka.” Hiyo ndio maana ya maneno Yake:
لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ
“Macho hayamzunguki na Yeye ndiye anayazunguka macho yote.”[5]
Kuhusu makanusho matupu hakuna matapo ndani yake tofauti na anavyoonelea al-Khaliyliy na maimamu wake Jahmiyyah, Mu´tazilah na Imaamiyyah katika mlango huu.
[1] Uk. 68
[2] 06:103
[3] 04:122
[4] 06:103
[5] 06:103
Mhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ar-Radd al-Qawiym, uk. 99-100
Imechapishwa: 14/01/2017
https://firqatunnajia.com/ibn-abbaas-na-qataadah-kuhusu-macho-kumdiriki-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)