Swali: Ni ipi hukumu ya swalah ya ´Iyd? Je, mtu anailipa ikimpita?
Jibu: Kilicho dhahiri ni kwamba swalah ya ´Iyd ni faradhi kwa kila mmoja. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameiamrisha. Ikimpita mtu basi hailipi. Jambo la kuilipa halikuthibiti. Hilo ni tofauti na swalah ya ijumaa. Swalah ya ijumaa ikimpita mtu anatakiwa kuilipa. Lakini hata hivo hatumwambii alipe swalah ileile, badala yake tunamwambia aswali Dhuhr. Hilo ni kwa sababu wakati huu ni ima ijumaa au Dhuhr. Hivyo ijumaa ikimpita badala yake aswali Dhuhr.
Kuhusu swalah ya ´Iyd imewekwa katika Shari´ah kwa njia ya mkusanyiko. Akipata mkusanyiko huu aswali. Asipopata mkusanyiko huu asilipe.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawa (16/214)
- Imechapishwa: 14/06/2018
Swali: Ni ipi hukumu ya swalah ya ´Iyd? Je, mtu anailipa ikimpita?
Jibu: Kilicho dhahiri ni kwamba swalah ya ´Iyd ni faradhi kwa kila mmoja. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameiamrisha. Ikimpita mtu basi hailipi. Jambo la kuilipa halikuthibiti. Hilo ni tofauti na swalah ya ijumaa. Swalah ya ijumaa ikimpita mtu anatakiwa kuilipa. Lakini hata hivo hatumwambii alipe swalah ileile, badala yake tunamwambia aswali Dhuhr. Hilo ni kwa sababu wakati huu ni ima ijumaa au Dhuhr. Hivyo ijumaa ikimpita badala yake aswali Dhuhr.
Kuhusu swalah ya ´Iyd imewekwa katika Shari´ah kwa njia ya mkusanyiko. Akipata mkusanyiko huu aswali. Asipopata mkusanyiko huu asilipe.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawa (16/214)
Imechapishwa: 14/06/2018
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-swalah-ya-iyd-na-inalipwa-ikimpita-mtu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)