Hukumu ya mwenye kusema kuwa dini haina uhusiano wowote na kazi

Swali: Tunasikia baadhi ya maneno yanayojirudirudi kutoka kwa baadhi ya wasimamizi kwamba kazi ni kazi na dini haina uhusiano wowote na kazi.

Jibu: Maneno haya ni batili. Ni vipi dini haina uhusiano na kazi? Dini ndio kila kitu. Dini ina mafungamano na kila kitu kuanzia katika kazi za watu, nyumba zao, uraisi wao, uongozi wao na mambo mengine yote. Dini ndio msingi wa kila kitu. Kazi inatakiwa iwe kwa mujibu wa mfumo wa dini. Mja anapaswa kuusalimisha uso wake kwa Allaah katika mambo yote:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً

”Enyi walioamini! Ingieni katika Uislamu kikamilifu.”[1]

Bi maana Uislamu mzima. Ni lazima kwa mtu aingie katika Uislamu yeye wote na ajifungamanishe na Uislamu katika kila kitu. Haijuzu kukwepa chochote. Ni lazima kuyapima matendo na maneno ya viongozi na wenye kuongozwa, waume kwa wake, watu kwa majini kwa mizani ya Shari´ah. Yale yanayoafikiana nayo yanachukuliwa na yale yanayotofautiana nayo yanarudishwa nyuma kwa mwenye nayo.

Yule mwenye kusema kuwa dini haina mafungamano yoyote na kazi anatakiwa kuambiwa atubie. Akitubia ni sawa na vinginevyo anauawa hali ya kuwa ni kafiri. Tunamuomba Allaah afya.

[1] 02:208

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa ad-Duruus https://binbaz.org.sa/fatwas/3683/%D8%AD%D9%83%D9%85-%D9%85%D9%86-%D9%8A%D9%82%D9%88%D9%84-%D9%84%D8%A7-%D8%AF%D8%AE%D9%84-%D9%84%D9%84%D8%AF%D9%8A%D9%86-%D9%81%D9%8A-%D8%A7%D9%84%D9%88%D8%B8%D9%8A%D9%81%D8%A9
  • Imechapishwa: 07/03/2020