Hukumu ya kumwambia maiti “Ee fulani! Niponye!”?

Swali: Mtu akimwita walii ambaye ni maiti kwa kumwambia:

“Ee fulani! Niponye!”

Je, hii inahesabika ni shirki kubwa?

Jibu: Haina shaka. Hii ndio shirki kubwa. Anaomba ponyo kutoka kwa maiti. Lau angelikuwa ni kiumbe yuko hai tungeliweza kusema kuwa pengine anakusudia amtibu. Lakini huyu ni maiti kisha unasema akuponye? Hili liko wazi ya kuwa ni shirki kubwa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (14) http://alfawzan.af.org.sa/node/2057
  • Imechapishwa: 25/04/2017