Swali: Mwanamke mjamzito anatokwa na damu. Ni ipi hukumu ya swalah zake na swawm yake? Je, aache kuswali na kufunga?
Jibu: Mwenye mimba akitokwa na damu, basi damu hiyo ni fasidi na sio hedhi. Hivyo aswali na swalah yake ni sahihi. Afunge na funga yake ni sahihi. Ni halali kwa mume wake yale ambayo ni halali kwake wakati anapokuwa hana damu hii. Kwa sababu damu hii wanachuoni wanaiita kuwa ni damu ´fasidi`.
Lakini asitawadhe kwa ajili ya kuswali isipokuwa baada ya kuingia wakati wa swalah hiyo. Isipokuwa swalah za sunnah wakati atapotaka kuswali basi atawadhe. Haijalishi kitu ni wakati gani mbali na zile nyakati zilizokatazwa. Kuhusu swalah za faradhi asitawadhe isipokuwa baada ya kuingia wakati. Hapa ni pale ambapo damu itakuwa ni yenye kuendelea. Ama ikiwa ni yenye kukatika na akatawadha na asitokwe na kitu mpaka ukaingia wakati wa swalah, basi aswali swalah yake na hakuna neno juu yake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (54) http://binothaimeen.net/content/1220
- Imechapishwa: 01/09/2019
Swali: Mwanamke mjamzito anatokwa na damu. Ni ipi hukumu ya swalah zake na swawm yake? Je, aache kuswali na kufunga?
Jibu: Mwenye mimba akitokwa na damu, basi damu hiyo ni fasidi na sio hedhi. Hivyo aswali na swalah yake ni sahihi. Afunge na funga yake ni sahihi. Ni halali kwa mume wake yale ambayo ni halali kwake wakati anapokuwa hana damu hii. Kwa sababu damu hii wanachuoni wanaiita kuwa ni damu ´fasidi`.
Lakini asitawadhe kwa ajili ya kuswali isipokuwa baada ya kuingia wakati wa swalah hiyo. Isipokuwa swalah za sunnah wakati atapotaka kuswali basi atawadhe. Haijalishi kitu ni wakati gani mbali na zile nyakati zilizokatazwa. Kuhusu swalah za faradhi asitawadhe isipokuwa baada ya kuingia wakati. Hapa ni pale ambapo damu itakuwa ni yenye kuendelea. Ama ikiwa ni yenye kukatika na akatawadha na asitokwe na kitu mpaka ukaingia wakati wa swalah, basi aswali swalah yake na hakuna neno juu yake.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (54) http://binothaimeen.net/content/1220
Imechapishwa: 01/09/2019
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-damu-inayomtoka-mjamzito/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)