Swali: Inajuzu kupaka rangi sehemu ya nywele kama kwa mfano mtu akapaka ncha au zile nywele zilizoko juu peke yake?
Jibu: Ikiwa kupaka rangi nywele ni kwa rangi nyeusi basi hakika Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amelikataza hilo pale alipoamrisha kuzibadilisha mvi na mtu ajiepushe na rangi nyeusi:
“Zibadilisheni mvi hizi na jiepusheni na [rangi] nyeusi.”
Isitoshe kumepokelewa makemeo juu ya yule mwenye kufanya hivi. Ni dalili inayothibitisha uharamu wa kuzibadilisha nywele kwa rangi nyeusi.
Ama kuzibadilisha kwa rangi nyingine kimsingi ni kwamba inafaa. Isipokuwa ikiwa ni kwa kujifananisha na wanawake wa kikafiri au watenda madhambi. Itakuwa ni haramu kwa upande huo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni katika wao.”
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/120)
- Imechapishwa: 28/06/2017
Swali: Inajuzu kupaka rangi sehemu ya nywele kama kwa mfano mtu akapaka ncha au zile nywele zilizoko juu peke yake?
Jibu: Ikiwa kupaka rangi nywele ni kwa rangi nyeusi basi hakika Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amelikataza hilo pale alipoamrisha kuzibadilisha mvi na mtu ajiepushe na rangi nyeusi:
“Zibadilisheni mvi hizi na jiepusheni na [rangi] nyeusi.”
Isitoshe kumepokelewa makemeo juu ya yule mwenye kufanya hivi. Ni dalili inayothibitisha uharamu wa kuzibadilisha nywele kwa rangi nyeusi.
Ama kuzibadilisha kwa rangi nyingine kimsingi ni kwamba inafaa. Isipokuwa ikiwa ni kwa kujifananisha na wanawake wa kikafiri au watenda madhambi. Itakuwa ni haramu kwa upande huo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni katika wao.”
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/120)
Imechapishwa: 28/06/2017
https://firqatunnajia.com/hukum-ya-wanawake-kupaka-sehemu-ya-nywle-za-kichwani-rangi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)