Swali: Waislamu wengi wanasema kuwa Allaah Yuko kila mahala…

Jibu: Tunamuomba Allaah afya. Sio waislamu wengi na himdi zote ni Zake Allaah. Hili ni kundi potevu lililopotea ambalo ni Huluuliyyah. Hii ni kufuru. Asiyemtakasa Allaah na sehemu za taka na anapinga kuweko Kwake juu ya ´Arshi juu ya mbingu zote, huyu ni kafiri na tunaomba kinga kwa Allaah. Huyu ni Huluuliy kafiri. Waislamu wengi hawana ´Aqiydah hii. Hii ni ´Aqiydah maalum ya Huluuliyyah na wanajulikana.

Swali: Je, wana dalili katika Kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):

فَأَيْنَمَا تُوَلُّوا فَثَمَّ وَجْهُ اللَّـهِ

“… basi popote mnapogeuka kuna Uso wa Allaah.” (02:115)

Jibu: Hili linahusiana na swalah katika Qiblah. Hili linahusiana na Qiblah. Anakuwa mbele ya mwenye kuswali na wakati huo huo Yuko juu ya mbingu na juu ya ´Arshi (Subhaanahu wa Ta´ala).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (47) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1432-04-08.mp3
  • Imechapishwa: 16/11/2014