Kuna ambao wanawafanya Salaf kuwa ni wajinga na wanawapuuza wanasema:

“Salaf ni wanaume na sisi pia ni wanaume.”

Wanasema vilevile:

“Ni sawa kwetu kuzua mambo. Sio lazima kwetu kuwafuata Salaf na maoni yao.”

Huu ni upotevu. Huku ni kukata mafungamano kati ya [watu wa] mwisho wa Ummah huu na wa mwanzo wao. Mwisho wa Ummah huu ukikatwa na wa mwisho wao basi Ummah unaangamia. Haya ndio makusudio yao. Wanachotaka ni kuuangamiza Ummah. Ndio maana wakawa wamekuja kwa njama hizi: kukata mwisho wa Ummah huu na wa mwanzo wao.

Leo kuna wenye kutahadharisha na madhehebu ya Salaf. Vilevile wanatadharisha kurejelea maoni yao. Wanasema kwamba ni zama zilizopita na kwamba karne zilizopota na wakati huo huo wanatadharisha juu yale waliyokuwemo Salaf na wanasisitiza kuzua mambo katika dini.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Sharh-is-Sunnah, uk. 32
  • Imechapishwa: 23/10/2017