Kuna mwanafunzi mmoja wa al-Hajuuriy, ambaye ni Husayn al-Hatwiybiy, alienda Tanzania kwa muda wa siku arobaini. Watanzania wakamkirimu kwa ikramu kubwa. Aliporudi akaandika kitabu chenye kichwa cha khabari “Arba´uuna yauman fiy Tanzaanyah”[1]. Ndani yake akataja aliyoyaona Tanzania na akataja vilevile uharibifu wa kimaadili unaofanywa na baadhi ya wasichana huko Tanzania. Hii ndio shukurani na kuwasifu kwake! Kuna ndugu yangu mmoja (ambaye yuko na jamaa zake huko Tanzania) alinieleza ya kwamba watanzania walisoma kitabu hichi ambapo wakasema:

“Watu hawa hawatorudi kwetu kabisa.”

[1] Tazama http://hateeby.com/?p=1715

  • Mhusika: Shaykh Abu ´Ammaar ´Aliy al-Hudhayfiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://m-noor.com/showthread.php?p=33728
  • Imechapishwa: 12/02/2017