Imaam Ahmad bin ´Aliy al-Maqriyziy anasema:

“[Katika maneno ya ulimi ni…] … kuuhifadhi na kubainisha upotofu wa watu wa Bid´ah wanaomkhalifu…”

Kubainisha upotofu wa watu wa Bid´ah wanaomkhalifu. Hili ni wajibu. Hatuwezi kunyamazia Bid´ah na kuacha watu kila mmoja na matamanio yake, ´Aqidah yake, mwekeleo wake kama jinsi leo invyochochewa kwenye magazeti na kwenginepo na kwenye ndimi za wajinga na wakanamungu. Wanataka munkari usikatazwe. Kusiamrishwe mema na wala kusikatazwe maovu na kuwaacha watu kwa waliomo. Wanataka munkari usikatazwe. Kusiamrishwe mema na wala kusikatazwe maovu na waachwe watu kwa waliomo. Kwa kuwa hili linafarikisha waislamu wanasema hivo. Ni kweli linafarakanisha waislamu. Asiyetaka kheri mwache atengane nasi. Tunapenda tu watu wenye kheri. Ama mtu mwenye shari, tunataka awe mbali nasi. Hatutaki kuwa naye.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://alfawzan.ws/sites/default/files/tg–1431-11-19.mp3
  • Imechapishwa: 09/04/2022