Hapana neno kwenda kutalii miji ya Kiislamu

Swali: Inajuzu kusafiri hali ya kutalii kwenda katika miji ya Kiislamu?

Jibu: Ndio, hakuna ubaya. Hakuna neno mtu akaenda kutalii katika miji ya Kiislamu ikiwa hachelei juu ya nafsi yake, hachelei juu ya Mahaarim zake na wala hachelei juu ya dini yake. Nchi ya Kiislamu hakuna neno. Kilichokatazwa ni kwenda kutalii katika miji ya kishirikina na miji ya kikafiri ambayo wanachuoni wamethibitisha kuwa haijuzu kusafiri kwenda katika miji ya makafiri isipokuwa kwa sharti:

1 – Mtu awe na elimu itamkinga kutokamana na utata.

2 – Awe ni mtu mwenye dini ambayo itamkinga kutokamana na utata mambo ya matamanio.

3 – Iwe ni safari ya kipindi fulani kwa sababu haja kisha baada ya hapo arudi katika mji wake.

Ama ikiwa kutalii ni katika mji wa waislamu na sambamba na hilo mtu hachelei juu ya nafsi yake, ataidhihirisha dini yake na wala hachelei fitina juu ya nafsi yake hakuna neno.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://shrajhi.com.sa/fatawa/14/%D8%B4%D8%B1%D9%88%D8%B7-%D8%A7%D9%84%D8%B3%D9%8A%D8%A7%D8%AD%D8%A9-%D8%A7%D9%84%D8%AC%D8%A7%D8%A6%D8%B2-%D9%85%D9%86%D9%87%D8%A7-%D9%88%D8%A7%D9%84%D9%85%D9%85%D9%86%D9%88%D8%B9
  • Imechapishwa: 02/02/2020