Hapa ndipo itamlazimu msafiri kwenda kuswali ijumaa

Mtunzi amesema:

”´Umar amesema: ”Swalah ya ijumaa sio kikwazo chochote cha safari.” Abu ´Ubaydah alisafiri siku ya ijumaa. az-Zuhriy amepokea Hadiyth kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisafiri siku ya ijumaa.”

Yote hayo yamepokelewa kutoka kwa Ibn Abiy Shaybah[1] na ´Abdur-Razzaaq[2].

Upokezi kutoka kwa ´Umar umepokelewa kupitia njia mbili ambapo moja wapo ni Swahiyh. Nimeutaja katika ”adh-Dhwa´iyfah”[3].

Upokezi kutoka kwa Abu ´Ubaydah una cheni ya wapokezi iliokatika.

Katika Hadiyth ya az-Zuhriy kuna Swahabah anayekosekana katika cheni. Hata hivyo maana yake ni sahihi muda wa kuwa hasikii adhaana. Ikiwa anasikia adhaana basi itamlazimu kwenda katika swalah ya ijumaa na Allaah ndiye mjuzi zaidi.

[1] al-Musannaf (2/105-106).

[2] al-Musannaf (3/250-251).

[3] 219.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tamaam-ul-Minnah, uk. 320
  • Imechapishwa: 29/01/2021