Ee dada wa Kiislamu! Tambua kwamba wale wanachuoni waliokujuzishia kuonyesha uso – pamoja na kwamba maoni yao ni dhaifu – lakini wameliwekea sharti ya kuaminika na fitina. Fitina si yenye kuaminika na khaswa katika zama hizi ambazo msukumo wa kidini kwa wanaume na wanawake umekuwa mdogo, haya imekuwa ndogo, walinganizi wa fitina wamekuwa wengi, wanawake wametafanuni kwa kuweka aina mbalimbali za mapambo kwenye nyuso zao, mambo ambayo yanaita katika fitina. Hivyo basi dada wa Kiislamu! Tahadhari kutokamana na hayo. Lazimiana na Hijaab itayokukinga kutokamana na fitina kwa idhini ya Allaah. Hakuna mwanachuoni yeyote wa Kiislamu, tokea hapo zamani hadi hii leo, ambaye anawajuzishia wanawake hawa waliofitiniwa yale waliyotumbukia ndani yake hii leo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tanbiyhaat ´alaa Ahkaam Takhtasswu bil-Mu´minaat, uk. 52
  • Imechapishwa: 16/11/2019