Swali: Kuna baadhi ya wanafunzi wanaosema kuwa Bid´ah zinatofautiana; kuna Bid´ah zenye kukufurisha, Bid´ah zenye kumtia mtu katika dhambi na Bid´ah zilizo chini ya hapo na kwamba hii ya mwisho imechukizwa na haikuharamishwa…

Jibu: Hapana, imeharamishwa. Kila Bid´ah ni yenye kuharamishwa. Hakuna Bid´ah iliyochukizwa. Maneno haya si sahihi:

“Nakutahadharisheni na mambo yaliyozuliwa. Kwani hakika kila Bid´ah ni upotevu.”

Hawa wanasema kuwa imechukizwa tu na sio upotevu?

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (79) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-9-2-1439-01.mp3
  • Imechapishwa: 05/03/2018