Hajaawirah wana mikhalafa mingi na wanachuoni wengi kabisa na hawana mukhalafa hata mmoja na al-Hajuuriy. Ni kama ambavyo al-Ikhwaan al-Muslimuun wana mikhalafa mingi na wanachuoni wengi na hawana mukhalafa hata mmoja na Hasan al-Bannaa. Hasan al-Bannaa ndio msingi na yanachukuliwa maneno ya wengine pale ambapo yatakuwa yameafikiana na msingi huu. Vivyo hivyo ndivyo walivyo wafuasi wa al-Hajuuriy. al-Hajuuriy ndio msingi na maneno ya wanachuoni wengine yanachukuliwa pale yatapokuwa ni yenye kuafikiana na msingi huu. Tunamuomba Allaah usalama na afya.

Hajaawirah siku zote utawaona ni wenye kutumia hoja wasia wa mwalimu wetu ambaye ni Shaykh Muqbil (Rahimahu Allaah) juu ya al-Hajuuriy[1] na alivyoacha anausia yeye ndio abaki katika kituo na kwamba hawako radhi ateremke kutoka juu ya kiti hichi. Kutumia hoja kwa wasia huu inapokuja katika kitendo hichi cha zamani ni hoja ya yule ambaye haelewi kitu kutoka katika Qur-aan na Sunnah na wala hakuielewa Salafiyyah.

Enyi watu! Nionyesheni uko wapi wasia wa Shaykh katika vitabu vyake alipoandika kwamba mumfuate al-Hajuuriy katika batili? Uko wapi wasia wa Shaykh katika vitabu vyake alipoandika kuwa na ushabiki kwake hata kama hilo litapelekea kuwaangusha wanachuoni wengine wote na abaki yeye peke yake?

[1] Tazama https://firqatunnajia.com/mapendekezo-ya-al-waadiiy-kwa-al-hajuuriy/

  • Mhusika: Shaykh Abu ´Ammaar ´Aliy al-Hudhayfiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://m-noor.com/showthread.php?p=33728
  • Imechapishwa: 28/01/2017