Haijuzu kuchukua elimu kutoka vitabuni

Swali: Kuna ambao wanasema kuwa mtu anaweza kutafuta elimu kupitia vitabu vilivyoshereheshwa na kwa hivyo sio lazima ahudhurie kwa wanachuoni na kuchukua elimu kutoka kwao moja kwa moja. Je, maneno haya ni sahihi?

Jibu: Huu ni upotevu. Haijuzu kuchukua elimu kutoka vitabuni. Ni lazima kukaa kwa wanachuoni na kuwasomea vitabu na wao washereheshe. Huku ndio kusoma.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (79) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-9-2-1439-01.mp3
  • Imechapishwa: 09/03/2018