Imaam an-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
21- Abu ‘Amr, vilevile imesemekana kuwa [anaitwa] Abu ‘Amrah Sufyaan bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza: “Nilisema: “Ee Mtume wa Allaah! Nieleze kitu juu ya Uislamu ambacho sintomuuliza mtu yeyote zaidi yako.” Akamwambia: “Sema: “Namuamini Allaah”, kisha uwe na msimamo.”
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Sema “Namuamini Allaah.”
Kama tulivyotangulia kusema ya kwamba imani ni: kauli, matedno na I´tiqaad. Akisema:
“Namuamini Allaah.”
Bi maana atakuwa ameamini I´tiqaad sahihi na ametenda matendo sahihi na mema yaliyoafikiana na Sunnah na akawa ni mwenye kumtakasia nia Allaah (Jalla wa ´Alaa). Vilevile amezungumza na kutamka Anayoyapenda Allaah (Jalla wa ´Alaa).
Kwa hivyo, maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Namuamini Allaah.”
Kunaingia ndani yake maneno, matendo na I´tiqaad. Ndani ya wasia huu kumeingia dini yote. Kwa sababu alisema:
“Nieleze kitu juu ya Uislamu ambacho sintomuuliza yeyote zaidi yako.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Sintomuuliza yeyote baada yako.”
Akamwambia:
“Sema: “Namuamini Allaah.”
- Mhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 305
- Imechapishwa: 14/05/2020
Imaam an-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
21- Abu ‘Amr, vilevile imesemekana kuwa [anaitwa] Abu ‘Amrah Sufyaan bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza: “Nilisema: “Ee Mtume wa Allaah! Nieleze kitu juu ya Uislamu ambacho sintomuuliza mtu yeyote zaidi yako.” Akamwambia: “Sema: “Namuamini Allaah”, kisha uwe na msimamo.”
Maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Sema “Namuamini Allaah.”
Kama tulivyotangulia kusema ya kwamba imani ni: kauli, matedno na I´tiqaad. Akisema:
“Namuamini Allaah.”
Bi maana atakuwa ameamini I´tiqaad sahihi na ametenda matendo sahihi na mema yaliyoafikiana na Sunnah na akawa ni mwenye kumtakasia nia Allaah (Jalla wa ´Alaa). Vilevile amezungumza na kutamka Anayoyapenda Allaah (Jalla wa ´Alaa).
Kwa hivyo, maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Namuamini Allaah.”
Kunaingia ndani yake maneno, matendo na I´tiqaad. Ndani ya wasia huu kumeingia dini yote. Kwa sababu alisema:
“Nieleze kitu juu ya Uislamu ambacho sintomuuliza yeyote zaidi yako.”
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Sintomuuliza yeyote baada yako.”
Akamwambia:
“Sema: “Namuamini Allaah.”
Mhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 305
Imechapishwa: 14/05/2020
https://firqatunnajia.com/hadiyth-sema-namuamini-allaah-kisha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)