Funga na chapa kazi zako za kila siku

Kadhalika mtu akifunga basi ni lazima kwake kutekeleza majukumu yake. Miongoni mwa majukumu ya mtu ni kazi. Ni mamoja ni kazi ya kiserikali kama mfano askari. Ni lazima kwa mtu kutekeleza kazi yake wakati wa kazi anaotakiwa kufanya hivo. Tena anatakiwa atekeleze kazi yake kwa nia safi. Hatakiwi kuchelewa wala kuona uzito. Jengine ni kwamba akija kazini ni lazima anatakiwa kutimiza kazi anayotakiwa kufanya. Asije tu pale kazini kuhudhurisha nafsi yake lakini hafanyi kazi. Sivyo hivyo. Ni lazima afanye kazi na atumie wakati huu juu ya yale aliyoombwa kufanya ikiwa ni pamoja na kazi unayotakiwa kufanya. Hili ni jambo la wajibu.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://shrajhi.com.sa/uploads/rmadhan_02.mp3
  • Imechapishwa: 09/05/2019