Fawziy al-Asharriy anaishi kati ya Raafidhwah na Suufiyyah. Katika maisha yake yote mpaka hii leo watu hawajapatapo kuona wala kusikia ana msimamo mtukufu wa ki-Suuniy ambapo anainusuru Sunnah na kuwavunja watu wa Bid´ah na wapotevu. Yuko namna hiyo kwa sababu yuko pamoja nao dhidi ya Ahl-us-Sunnah au ni mwoga?
Juhudi kubwa tunayoiona kutoka kwake anaiweka tu dhidi ya Ahl-us-Sunnah kwa uongo, ujinga na upotoshaji. Ameandika vitabu vine vikiwa na kichwa cha khabari ”ar-Ru´uud as-Swawaa´iqiyyah”, ”al-Burkaan”, ”al-Qaasimah al-Khafidhwah” na vyote ni uongo mtupu na kumfanyia khiyana Rabiy´ na nduguze katika Ahl-us-Sunnah.
Hatuoni nashati yake isipokuwa kuwa dhidi ya Hadiyth zilizomo katika “as-Swahiyh” ya Muslim kwa mfano Hadiyth kuhusu kufunga siku ya ´Arafah na kuhusu uombezi. Ameandika vitabu viwili juu ya hilo. Anaeneza uvumi juu ya “as-Swahiyh” ya Imaam Muslim na kuituhumu kwamba imejaa Hadiyth nyingi mbovu (شاذ).
Uko wapi wewe ukilinganisha na wanachuoni wa Ahl-us-Sunnah ambao wanabainisha upotevu wa Raafidhwah ambapo mmoja wao ni Muhammad Maalullah al-Bahrayniy (Rahimahu Allaah) ambaye aliweka juhudi kubwa katika kubainisha upotevu na uchafu wa Raafidhwah.
Uko wapi wewe na Ruduud za Ahl-us-Sunnah kwa Suufiyyah na waabudu makaburi?
Uko wapi wewe na vitabu vinavyoitetea “as-Swahiyh” ya Muslim na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuraddi mashambulizi yake?
Uko wapi wewe na Ruduud walizotwangwa Haddaadiyyah ambao wanawapiga vita Ahl-us-Sunnah kwa kutumia jina la Ahl-us-Sunnah? Ni vipi utawaraddi ilihali wewe ni mmoja katika viongozi na walinzi wao?
Wewe uko wapi na wale Murji-ah wa kikweli ambao unawatumia kwa kuwapiga vita Ahl-us-Sunnah na kuwasingizia na kuwatupia tuhuma mbaya?
Uko wapi, wewe Khalafiy ambaye unataka kuigeuza jihadi dhidi ya wapotevu, ukilinganisha na wale Khawaarij wa kale na wa sasa?
Woga wasaliti wasiishi!
- Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kashf Akaadhiyb wa Tahriyfaat wa Khiyaanaat Fawziy al-Bahrayniy, uk. 15-16
- Imechapishwa: 09/10/2016
Fawziy al-Asharriy anaishi kati ya Raafidhwah na Suufiyyah. Katika maisha yake yote mpaka hii leo watu hawajapatapo kuona wala kusikia ana msimamo mtukufu wa ki-Suuniy ambapo anainusuru Sunnah na kuwavunja watu wa Bid´ah na wapotevu. Yuko namna hiyo kwa sababu yuko pamoja nao dhidi ya Ahl-us-Sunnah au ni mwoga?
Juhudi kubwa tunayoiona kutoka kwake anaiweka tu dhidi ya Ahl-us-Sunnah kwa uongo, ujinga na upotoshaji. Ameandika vitabu vine vikiwa na kichwa cha khabari ”ar-Ru´uud as-Swawaa´iqiyyah”, ”al-Burkaan”, ”al-Qaasimah al-Khafidhwah” na vyote ni uongo mtupu na kumfanyia khiyana Rabiy´ na nduguze katika Ahl-us-Sunnah.
Hatuoni nashati yake isipokuwa kuwa dhidi ya Hadiyth zilizomo katika “as-Swahiyh” ya Muslim kwa mfano Hadiyth kuhusu kufunga siku ya ´Arafah na kuhusu uombezi. Ameandika vitabu viwili juu ya hilo. Anaeneza uvumi juu ya “as-Swahiyh” ya Imaam Muslim na kuituhumu kwamba imejaa Hadiyth nyingi mbovu (شاذ).
Uko wapi wewe ukilinganisha na wanachuoni wa Ahl-us-Sunnah ambao wanabainisha upotevu wa Raafidhwah ambapo mmoja wao ni Muhammad Maalullah al-Bahrayniy (Rahimahu Allaah) ambaye aliweka juhudi kubwa katika kubainisha upotevu na uchafu wa Raafidhwah.
Uko wapi wewe na Ruduud za Ahl-us-Sunnah kwa Suufiyyah na waabudu makaburi?
Uko wapi wewe na vitabu vinavyoitetea “as-Swahiyh” ya Muslim na Sunnah za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuraddi mashambulizi yake?
Uko wapi wewe na Ruduud walizotwangwa Haddaadiyyah ambao wanawapiga vita Ahl-us-Sunnah kwa kutumia jina la Ahl-us-Sunnah? Ni vipi utawaraddi ilihali wewe ni mmoja katika viongozi na walinzi wao?
Wewe uko wapi na wale Murji-ah wa kikweli ambao unawatumia kwa kuwapiga vita Ahl-us-Sunnah na kuwasingizia na kuwatupia tuhuma mbaya?
Uko wapi, wewe Khalafiy ambaye unataka kuigeuza jihadi dhidi ya wapotevu, ukilinganisha na wale Khawaarij wa kale na wa sasa?
Woga wasaliti wasiishi!
Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kashf Akaadhiyb wa Tahriyfaat wa Khiyaanaat Fawziy al-Bahrayniy, uk. 15-16
Imechapishwa: 09/10/2016
https://firqatunnajia.com/fawziy-ni-nani/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)