Swali: Mimi namwamrisha mke wangu kuvua suruwali. Lakini hata hivyo anakataa na kusema kwamba hakuna yeyote aliye pamoja na sisi. Nifanye nini? Je, nimhame wakati wa kulala? Nielekeze na Allaah atakujaze kheri. Je, ninapata dhambi baada ya kumnasihi?

Jibu: Hiki ni kitu rahisi. Wewe ndiye msimamizi juu yake. Mpokonye suruwali hiyo na uichome moto mbele yake na huku anaitazama. Badala yake avae kanzu na nguo zenye kumsitiri. Vipi atakushinda? Wewe ni mwanaume au mwanamke?

وَاللَّاتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ

“Wale ambao mnakhofu uasi kutoka kwao, basi wanasihini na wahameni katika malazi na wapigeni.” (04:34)

Mwanamke pindi (´Azza wa Jall) aliposema:

وَإِنِ امْرَأَةٌ خَافَتْ مِن بَعْلِهَا نُشُوزًا أَوْ إِعْرَاضًا فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِمَا أَن يُصْلِحَا بَيْنَهُمَا صُلْحًا

“Na ikiwa mke atachelea kutoka kwa mumewe uonevu wa ndoa au kutengwa, basi hakuna neno juu yake wakisikilizana kati yao kwa suluhu.” (04:128)

Hakusema mwanamke ampige mwanaume. Lakini inapokuja kwa mwanaume alisema:

وَاللَّاتِي تَخَافُونَ نُشُوزَهُنَّ فَعِظُوهُنَّ وَاهْجُرُوهُنَّ فِي الْمَضَاجِعِ وَاضْرِبُوهُنَّ

“Wale ambao mnakhofu uasi kutoka kwao, basi wanasihini na wahameni katika malazi na wapigeni.”

Wewe ndiye una usimamizi juu yake. Angelikuwa halipendi vazi hili basi asingeanza kubishana na wewe. Kwa sababu kama ingelikuwa ni kwa ajili yako, anaweza kitandani akakuvulia nguo zote uchi kabisa na asivae si suruwali, jinzi wala kitu kingine. Juu yenu mkajifunika shuka ili msibaki mkiwa uchi. Ikiwa jambo hili linaruhusu kwa mke kuna faida gani ya kuvaa suruwali? Mimi nakwambia: muombe Allaah msaada dhidi yake na uchukue suruwali hiyo na uichome moto na yeye – Allaah akitaka – atanyenyekea haki.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (56) http://binothaimeen.net/content/1270
  • Imechapishwa: 06/07/2020