Swali: Mtu akimuombea du´aa mbaya ambaye amemdhulumu au ambaye anadhihirisha waziwazi baadhi ya madhambi makubwa kwamba Allaah awaangamize watoto wake au awafanye kuwa wagonjwa – je, du´aa mfano wa hii inakubaliwa ingawa wao hawakumshambulia wala hawakumdhulumu?
Jibu: Haifai kwake kufanya hivo. Haitakikani kwa mtu kuomba dhidi yake. Bali anatakiwa kumuombea uongofu. Ambaye kamdhulumu anapaswa kumsamehe. Akimsamehe ndio bora. Amesema (Ta´ala):
وَأَن تَعْفُوا أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ
“Mkisamehe ni ukaribu zaidi wa kumcha Allaah.”[1]
فَمَنْ عَفَا وَأَصْلَحَ فَأَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ
”Atakayesamehe na akatengeneza, basi ujira wake uko kwa Allaah.”[2]
Pengine wakati wa kuomba dhidi ya aliyemdhulumu akaongeza katika du´aa yake. Yule mwenye kuombewa dhidi yake akachukua ziada kutoka kwake [siku ya Qiyaamah].
[1] 02:237
[2] 4240
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (21)
- Imechapishwa: 12/09/2021
Swali: Mtu akimuombea du´aa mbaya ambaye amemdhulumu au ambaye anadhihirisha waziwazi baadhi ya madhambi makubwa kwamba Allaah awaangamize watoto wake au awafanye kuwa wagonjwa – je, du´aa mfano wa hii inakubaliwa ingawa wao hawakumshambulia wala hawakumdhulumu?
Jibu: Haifai kwake kufanya hivo. Haitakikani kwa mtu kuomba dhidi yake. Bali anatakiwa kumuombea uongofu. Ambaye kamdhulumu anapaswa kumsamehe. Akimsamehe ndio bora. Amesema (Ta´ala):
وَأَن تَعْفُوا أَقْرَبُ لِلتَّقْوَىٰ
“Mkisamehe ni ukaribu zaidi wa kumcha Allaah.”[1]
فَمَنْ عَفَا وَأَصْلَحَ فَأَجْرُهُ عَلَى اللَّـهِ
”Atakayesamehe na akatengeneza, basi ujira wake uko kwa Allaah.”[2]
Pengine wakati wa kuomba dhidi ya aliyemdhulumu akaongeza katika du´aa yake. Yule mwenye kuombewa dhidi yake akachukua ziada kutoka kwake [siku ya Qiyaamah].
[1] 02:237
[2] 4240
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (21)
Imechapishwa: 12/09/2021
https://firqatunnajia.com/duaa-mbaya-kwa-aliyekudhulumu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)