Swali: Mama yangu ni mgonjwa kwenye jicho lake. Daktari mmoja anamshauri kunywa mimea iliyochanganyikana na alcohol. Asipofanya hivo basi atalazimika kufanyiwa upasuaji. Je, inajuzu kwake kunywa?
Jibu: Alcohol ni uchawi. Haijuzu kujitibu kwa uchawi. Kuna madawa mengine:
“Allaah hakuteresha ugonjwa wowote isipokuwa ameteremsha vilevile dawa yake; amejua yule mwenye kujua na hakujua yule ambaye hakujua.”[1]
Apeleke suala lake kwa wenye uzoefu na watambuzi na amuombe Allaah du´aa (Subhaanahu wa Ta´ala) amponye.
[1] at-Twabaraaniy katika ”al-Mu´jam al-Awsatw” (3/75). Swahiyh kwa mujibu wa Ibn ´Abdil-Barr i ”at-Tamhiyd” (5/283).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (61) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20majid-%2029%20-0%206-1438.mp3
- Imechapishwa: 06/08/2017