Swali: Watu wawili waliingia na wakamkuta imamu katika Tashahhud ya mwisho. Bora wajiunge nao katika swalah au wasubiri mpaka kutolewe salamu na waswali swalah upya?
Jibu: Wakiwa wawili au watatu na wamekuja na kumkuta imamu katika Tashahhud basi wako na khiyari; wakitaka wanaweza kujiunga pamoja na imamu na wakitaka wanaweza kusubiri mpaka kutolewe salamu. Kwa sababu swalah imeisha na swalah haiwahiwi isipokuwa kwa Rak´ah moja. Kwa hiyo wako na khiyari. Ama akiwa ni mtu mmoja asisubiri. Ajiunge pamona na imamu. Asisemi kuwa eti anasubiri mpaka aje mwengine na huenda huyo mwingine asije. Wakiwa wawili au zaidi basi wako na khiyari. Akiwa ni mmoja ajiunge pamoja na imamu japokuwa ni katika Tashahhud ya mwisho. Asisubiri. Hapana shaka kwamba wanapata thawabu za kuswali kwa mkusanyiko. Lakini ule mkusanyiko wa kwanza una ubora wake.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
- Imechapishwa: 22/05/2019
Swali: Watu wawili waliingia na wakamkuta imamu katika Tashahhud ya mwisho. Bora wajiunge nao katika swalah au wasubiri mpaka kutolewe salamu na waswali swalah upya?
Jibu: Wakiwa wawili au watatu na wamekuja na kumkuta imamu katika Tashahhud basi wako na khiyari; wakitaka wanaweza kujiunga pamoja na imamu na wakitaka wanaweza kusubiri mpaka kutolewe salamu. Kwa sababu swalah imeisha na swalah haiwahiwi isipokuwa kwa Rak´ah moja. Kwa hiyo wako na khiyari. Ama akiwa ni mtu mmoja asisubiri. Ajiunge pamona na imamu. Asisemi kuwa eti anasubiri mpaka aje mwengine na huenda huyo mwingine asije. Wakiwa wawili au zaidi basi wako na khiyari. Akiwa ni mmoja ajiunge pamoja na imamu japokuwa ni katika Tashahhud ya mwisho. Asisubiri. Hapana shaka kwamba wanapata thawabu za kuswali kwa mkusanyiko. Lakini ule mkusanyiko wa kwanza una ubora wake.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (11) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191491#219817
Imechapishwa: 22/05/2019
https://firqatunnajia.com/bora-waswali-mkusanyiko-wao-upya-au-wajiunge-pamoja-na-imamu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)