Swali: Ni ipi hukumu ya kuuza mikanda na vitabu ambapo ndani yake kuna kuwatukana Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) au kuigawanya kwa watu ili waweze kusikiliza? Unamnasihi nini kwa anayefanya hivo?

Jibu: Kuuza mikanda hii au vitabu ambavyo vina kuwatukana Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) au baadhi yao, ni uuzaji wa batili. Hii ni bidhaa ya haramu. Ni wajibu kuivunja na kuichana. Thamani yake ni haramu. Kuieneza ni haramu. Lililo la wajibu ni kuivunja na kuichana.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (13) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_13.mp3
  • Imechapishwa: 19/06/2018