Basi halisimami kwa ajili ya Fajr

Swali: Nikiwa ni msafiri na ukaingia wakati wa swalah ya alfajiri. Dereva wa basi akakataa kusimama ili tuswali swalah ya Fajr mpaka pale atapopata kituo cha kutia mafuta ambapo nikachelea kuisha kwa muda wa swalah. Je, inafaa kwangu kuswali ndani ya basi na mimi nimeketi?

Jibu: Ndio. Swali kwa kuketi. Swali kwa kadri na hali yako ijapo kwa kuashiria.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (105) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/20-03-1441-H-%20igah.mp3