Baba hawi shahidi wa binti yake katika ndoa

Swali: Je, inajuzu baba wa mke kuwa shahidi katika ndoa?

Jibu: Hapana. Baba wa mke ni walii. Ni lazima kupatikane walii na mashahidi wawili.

“Hakuna ndoa isipokuwa mpaka kwa walii na mashahidi wawili waadilifu.”

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (68) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13864
  • Imechapishwa: 16/11/2014