Baba anaona kuwa inafaa na mtoto anaona kuwa haifai

Swali: Ikiwa kuna masuala ambayo wanazuoni wametofautiana ambapo baba anaona kuwa ni halali na mtoto wake anaona kuwa ni haramu. Baba akamwambia mtoto wake kwamba anamtaka afanye kitu hicho ambacho naona kuwa kinafaa. Hata hivyo mtoto anaona kuwa ni haramu. Afanye nini? Amtii au asimtii?

Jibu: Ikiwa baba na mtoto wote wawili wameshafikia ngazi ya Ijtihaad ya kielimu, kila mmoja katika wao ameshakuwa Mujtahid katika elimu, basi hapo ndipo maudhui hiyo itaangaliwa. Lakini pengine baba hajui hata kuswali na mtoto hajui kuswali. Ni vipi basi watatofautiana katika masuala ya kielimu? Kimsingi haijuzu kwao kuingia ndani ya masuala haya ya kielimu. Allaah (Ta´ala) amesema:

فَاسْأَلُواْ أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لاَ تَعْلَمُونَ

“Basi waulizeni wenye ukumbusho kama nyinyi hamjui.” (16:43)

Lakini ukiniletea baba ambaye ni Mujtahid na mtoto ambaye ni Mujtahid basi itakuwa ni vyema.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdullaah bin ´Abdir-Rahmaan al-Ghudayyaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa al-Usrah https://godian.af.org.sa/sites/default/files/2017-10/ftawa-osrh-godian.mp3
  • Imechapishwa: 20/09/2022