Baba anakhofia watoto kwenda msikitini anapokuwa hayuko nyumbani

Swali: Nikiwa sipo nyumbani wakati kunapoadhiniwa kwa ajili ya swalah ni wajibu kwa watoto wangu kwenda msikitini pamoja na kuwa barabarani kuna magari mengi yanayopita na watoto wangu bado hawajabaleghe na kuna khatari kwao?

Jibu: Wawakilishie mtu. Muwakilishe jirani au mtu mwengine awezaye kwenda nao. Wawakilishie mtu. Ni lazima waende msikitini. Ikiwa unachelea juu yao muwakilishe jirani yako, imamu wa msikiti au muadhini. Hawa wanaweza kusaidiana na wewe.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (83) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-15-3-1439-01.mp3
  • Imechapishwa: 12/01/2018