7- Wana ufuataji wa kichwa mchunga wa chuki na ushabiki wa upofu kwa watu ambao wanajulikana kwa Ahl-us-Sunnah kwa uongo, khiyana na dhuluma. Wanapenda na kuchukia kwa ajili ya watu hawa na batili zao. Sifa hii iko na Haddaadiyyah wa zamani na Haddaadiyyah wa sasa.

Pamoja na aibu hii wanawatuhumu Ahl-us-Sunnah kuwa na ushabiki na kufuata kipofu. Wanasema uongo. Ahl-us-Sunnah ni wenye kushikamana na mfumo wa Salaf pindi wanapohukumu na kutendea kazi Qur-aan na Sunnah. Wanawahukumu watu kwa Qur-aan na Sunnah kwa ufahamu wa Salaf; yale ambayo ni haki na ni yenye kuafikiana na Qur-aan na Sunnah wanayakubali na kuyasapoti na kuyanusuru na si vinginevyo.

Haddaadiyyah wa zamani wana misingi mingine vilevile ambayo nimeitaja katika makala “Manhaj-ul-Haddaadiyyah” ambayo niliieneza kabla ya Haddaadiyyah hawa wapya kujitokeza. Kuna uwezekano vilevile ikapatikana hata kwa hawa Haddaadiyyah wa hivi sasa, lakini hata hivyo wanaificha kwa Taqiyyah. Ni jambo linalowezekana kwao. Wana ufuataji wa kichwa mchunga na ushabiki wa upofu ulio na chuki kama tulivyosema ambao hata Ahl-ul-Bid´ah waliopindukia wanastahi kwao.

8- Sifa nyingine ambayo Haddaadiyyah hawa wa sasa wamewashinda Haddaadiyyah wa zamani ni kuwa na Taqiyyah inayoshinda Taqiyyah ya Raafidhwah. Upande mwingine Haddaadiyyah wa zamani walikuwa wadhahiri na wa wazi katika maneno na misimamo yao. Upande mwingine Haddaadiyyah wa sasa wanatumia msingi huu wa Raafidhwah.

9- Usiri na mikakati ya kujificha. Namna hii ndivyo wanavyowapiga vita Ahl-us-Sunnah na kutumia majina yasiyojulikana.

10- Uongo, khiyana na upotoshaji wa maneno kuyatoa mahala pake.

11- Mwenye kusema kuwa tofauti kati ya Ahl-us-Sunnah na Muji-ah al-Fuqahaa´ ni ya kimatamshi tu wanamtuhumu upotevu. Hili linapelekea kuwatuhumu vilevile Salaf, Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah na maimamu wa Salafiyyah Najd ambao pia wamesema hivo upotevu. Baya kuliko hilo ni kuwa wanamsemea uongo asiyesema hivo na halafu wanamfanyia Tabdiy´ na wanamkashifu kujengea juu ya uongo na uzushi wao.

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kashf Akaadhiyb wa Tahriyfaat wa Khiyaanaat Fawziy al-Bahrayniy, uk. 6-7
  • Imechapishwa: 09/10/2016