Swali: Kuna mtu aliacha swalah na swawm kwa miaka mingi. Je, azilipe baada ya kutubia?

Jibu: Tawbah inatosha. Atubu kwa Allaah na achunge swalah na swawm katika mustakabali. Kwa sababu kuacha swalah ni ukafiri. Pale alipoacha swalah kwa kukusudia alikuwa kafiri. Ni wajibu kwake kusilimu upya, ahifadhi swalah na atubu kwa Allaah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (86) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/NEW.lite_.mp3
  • Imechapishwa: 30/06/2018