Kila kigawanyo cha Tawhiyd kila dalili yake. Ikishakuwa kila kigawanyo kila dalili yake, basi inapata kujulikana kuwa ni jambo ambalo halikuzushwa kama wanavodai baadhi ya watu. Baadhi yao wamefikia mpaka kusema ya kwamba kuigawanya Tawhiyd vigawanyo hivi ni kama mfano wa imani ya utatu kwa manaswara – na tunaomba kinga kwa Allaah. Vigawanyo hivi vimechukuliwa kutoka kwenye Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama itavokuja huko mbele.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/26)
  • Imechapishwa: 07/06/2020