Swali: Inajuzu kwa mtu kuchinja ´Aqiyqah nje ya mji wake kwa sababu kuna mafakiri wengi huko?

Jibu: ´Aqiyqah na Udhhiyah vinatakiwa kuchinjwa majumbani. Visichinjwe mahala kwengine. Hii ndio Sunnah. Ikiwa unataka kuwapa swadaqah walio nje ya mji watumie pesa au chakula. Udhhiyah na ´Aqiyqah ni nembo ambazo hazitakiwi kufanywa pahala pengine.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (39) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighasah%20%208%20-%2011%20-%201436.mp3
  • Imechapishwa: 13/02/2017