Anaswali lakini anapata uzito kuacha sigara      

Swali: Mimi ni kijana ninayeswali swalah zote, lakini hata hivyo ninavuta sigara. Baada ya kuvuta sigara natubia, kisha narejea, kisha natubia, kisha narejea mara nyingi. Ninaogopa adhabu ya Moto. Nifanye nini? Natarajia utaniombea kuiacha na niwe katika watu wema na watengenezaji.

Jibu: Ninamuomba Allaah amsaidie kuacha na atujaalie sote kuwa katika watu wema. Kimbilia kuwa mwenye nguvu juu ya nafsi yako na jitenge mbali na wale wavutaji. Kwa sababu kuwa na ukaribu nao kutakuvutia kwao na kuvuta. Jitenge nao mbali, uchome zile sigara ulizonazo na umuombe Allaah (´Azza wa Jall) uthabiti akukinge kutokamana na ulinzi Wake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (05)
  • Imechapishwa: 02/05/2020