Anadaiwa Ramadhaan miaka kumi na nne iliyopita

Swali: Kuna mwanamke anadaiwa kulipa swawm ya mwezi wote wa Ramadhaan. Hayo ni kwa sababu hakufunga mwezi wa Ramadhaan takriban miaka kumi na nne iliyopita. Kuna mtu alimkumbusha kufunga masiku haya. Ni lipi la lazima kwake katika hali kama hii?

Jibu: Ni lazima kwake kulipa. Endapo alikuwa amesahau au mjinga na hakuwa anajua basi ni lazima kwake kulipa peke yake. Iwapo alikuwa anajua lakini hata hivyo akachukulia wepesi basi atalipa na atalisha kwa kila siku moja masikini kwa sababu ya kuchelewesha kwake.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (12) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=audioinfo&audioid=191546
  • Imechapishwa: 11/10/2019