Swali: Kuna mtu amesilimu baada ya kupita masiku kadhaa ya Ramadhaan. Je, ni lazima kwake kulipa masiku yaliyompita?
Jibu: Huyu hahitajii kulipa masiku yaliyompita. Kwa sababu kipindi hicho alikuwa ni kafiri. Kafiri hahitajii kulipa matendo mema yaliyompita. Allaah (Ta´ala) amesema:
قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوا إِن يَنتَهُوا يُغْفَرْ لَهُم مَّا قَدْ سَلَفَ
“Waambie wale waliokufuru kwamba wakikoma watasamehewa yaliyotangulia.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiwaamrisha wale wenye kusilimu kulipa swawm, swalah au zakaah zilizowapita. Lakini iwapo atasilimu katikati ya mchana ni lazima kujizuia na kuilipa siku hiyo au ajizuie na asilipe siku hiyo au haimlazimu kujizuia wala kulipa? Wanachuoni wametofautiana juu ya mambo haya. Maoni yenye nguvu ni kwamba analazimika kujizuia na kutoilipa siku hiyo kwa sababu ameingia miongoni mwa watu ambao wanawajibika, lakini halazimiki kuilipa siku hiyo kwa sababu kabla ya hapo hakuwa miongoni mwa watu wanaowajibika. Yeye ni kama mtoto ikiwa atabaleghe katikati ya mchana; atalazimika kujizuia siku hiyo na wala hatolazimika kuilipa. Hayo ndio maoni yaliyo na nguvu katika masuala haya.
[1] 08:38
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (19/96-97)
- Imechapishwa: 22/05/2019
Swali: Kuna mtu amesilimu baada ya kupita masiku kadhaa ya Ramadhaan. Je, ni lazima kwake kulipa masiku yaliyompita?
Jibu: Huyu hahitajii kulipa masiku yaliyompita. Kwa sababu kipindi hicho alikuwa ni kafiri. Kafiri hahitajii kulipa matendo mema yaliyompita. Allaah (Ta´ala) amesema:
قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوا إِن يَنتَهُوا يُغْفَرْ لَهُم مَّا قَدْ سَلَفَ
“Waambie wale waliokufuru kwamba wakikoma watasamehewa yaliyotangulia.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiwaamrisha wale wenye kusilimu kulipa swawm, swalah au zakaah zilizowapita. Lakini iwapo atasilimu katikati ya mchana ni lazima kujizuia na kuilipa siku hiyo au ajizuie na asilipe siku hiyo au haimlazimu kujizuia wala kulipa? Wanachuoni wametofautiana juu ya mambo haya. Maoni yenye nguvu ni kwamba analazimika kujizuia na kutoilipa siku hiyo kwa sababu ameingia miongoni mwa watu ambao wanawajibika, lakini halazimiki kuilipa siku hiyo kwa sababu kabla ya hapo hakuwa miongoni mwa watu wanaowajibika. Yeye ni kama mtoto ikiwa atabaleghe katikati ya mchana; atalazimika kujizuia siku hiyo na wala hatolazimika kuilipa. Hayo ndio maoni yaliyo na nguvu katika masuala haya.
[1] 08:38
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (19/96-97)
Imechapishwa: 22/05/2019
https://firqatunnajia.com/amesilimu-mchana-wa-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)