Swali: Kuna mtu amemjamii mke wake mchana wa Ramadhaan siku tatu kwa wakati mbalimbali. Mtu huyo hawezi kulipa. Kipi kinachomlazimu?

Jibu: Ni lazima kwake kutubu kwa Allaah. Ni maovu. Ni lazima kuacha mtumwa huru kwa kila siku moja; inakuwa watumwa tatu. Asipoweza afunge miezi sita; kila jimaa miezi miwili. Anapaswa afululize pale atapoweza kufanya hivo. Asipoweza hakuna kinachomlazimu. Anatakiwa ajitahidi pengine anaweza. Akiweza basi atafunga miezi miwili kwa kila jimaa. Sambamba na hilo ni lazima atubu kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa). Hayo yatabaki katika dhimma yake mpaka pale atakapoweza mpaka wakati atapofariki.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaad-Duruus https://binbaz.org.sa/fatwas/3727/%D9%85%D8%A7-%D8%AA%D8%B1%D8%AA%D9%8A%D8%A8-%D8%A7%D9%84%D9%83%D9%81%D8%A7%D8%B1%D8%A9-%D9%84%D9%85%D9%86-%D8%AC%D8%A7%D9%85%D8%B9-%D9%81%D9%8A-%D9%86%D9%87%D8%A7%D8%B1-%D8%B1%D9%85%D8%B6%D8%A7%D9%86
  • Imechapishwa: 19/05/2020