169- Nilimuuliza baba yangu kuhusu msafiri ambaye ameamka akiwa mbali na maji. Akiyaenda maji basi jua litamchomozea. Je, afanye Tayammum au ayaendee maji? Akajibu:

“Ayatafute maji mpaka pale atakapochelea kupitwa na swalah. Wakati anapochelea kuchomoza kwa jua basi afanye Tayammum na kuswali.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdullaah bin Ahmad bin Hanbal
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad (1/130-131)
  • Imechapishwa: 22/01/2021